HIGHLIGHTS: Yanga ilivyolazimishwa sare na St. Louis, Ushelisheli (21/02/2018)


Mabingwa wa Tanzania Bara Yanga SC imefanikiwa kusonga mbele katika raundi ya kwanza ya michuano ya klabu Bingwa barani Afrika baada ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya St. Louis ya Ushelisheli. Matokeo hayo ya mchezo wa leo uliopigwa katika dimba la Stade Linite nchini Ushelisheli, yameifanya Yanga ifuzu kwa jumla ya mabao 2-1, kufuatia ushindi wa bao 1-0 iliyoupata katika mchezo wa kwanza uliopigwa katika dimba la Taifa, Februari 10 mwaka huu. Katika mchezo wa leo uliokuwa ‘live’ Azam Sports, Yanga ndiyo waliotangulia kupata bao dakika ya 45 kupitia kwa Ibrahim Ajib aliyemalizia pasi ya Hassan Ramadhan Kessy, ikiwa ni sekunde chache kabla ya mapumziko.
SOURCE Azam TV


Download DJChokaUpDates Android Application Click >>> HERE 
TWITTER @DJChokaUpDates
INSTAGRAM @DJChokaUpDates

No comments

TUTUMIE UPDATES ZAKO KUPITIA
WhatsApp: +255 658 164282

Email: djchoka@gmail.com