Ukimuuliza Samatta Taifa Stars inahitaji kocha wa kigeni? atakujibu hivi

Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars Jumanne ya March 27 2018 ilicheza game yake ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya timu ya Congo DRC uwanja wa Taifa Dar es Salaam, mchezo ulimalizika kwa Taifa Stars kupata ushindi wa magoli 2-0, magoli yakifungwa na Mbwana Samatta dakika ya 74 na Shiza Kichuya dakika ya 85. Baada ya game AyoTV iliongea na nahodha wa Taifa Stars Mbwana Samatta aelezee game hiyo baada ya ushindi huo, ikiwa ni siku tano zimepita toka Taifa Stars wapoteza dhidi ya Algeria kwa magoli 4-1, Samatta ameuelezea mchezo huo na kueleza kuwa Tanzania inahitaji wachezaji wengi professional ili izidi kufanya vizuri.
SOURCE Millard Ayo
Download DJChokaUpDates Android Application Click >>> HERE
TWITTER @DJChokaUpDates
INSTAGRAM @DJChokaUpDates
FACEBOOK FANS PAGE>>> https://www.facebook.com/djchokaupdat
Post a Comment